Tip:
Highlight text to annotate it
X
(tarumbeta inapigwa)
Ninapenda hii.
(tarumbeta inapigwa)
Ahsante.
(kushangiolia na makofi)
Asante.
Nafikiri Congress inahitaji mojawapo ya hizi baragumu
(kicheko)
Inasikika vizuri sana.
Utadhani Louis Armstrong yupo hapa.
(kicheko)
Habari za mchana watu wote.
Ni heshima kubwa kwangu kuwa Accra,
Na kuzungumza mbele ya wawakilishi wa watu wa Gnana.
(kushangulia na makofi)
Ninashukuru sana kwa makaribisho niliyopewa,
vile vile Michelle na Malia, na Sasha Obama.
Historia ya Ghana ni kubwa, uhusianobaina ya nchi zetu mbili
ni imara, na ninaona fahari kwamba hii ni ziara yangu ya kwanza
katika nchi kusini ya Sahara nikiwa rais wa Marekani.
kushangilia na makofi)
Nataka kumshukuru Bibi Spika na wabunge wote
kwa kutukaribisha hapa leo.
Nataka kumshukuru rais Mills kwa uongozi wake wa ufanisi.
Kwa marais wa zamani-- Jerry Rawlings
rais wa zamani Kufuor; Makamu wa Rais;Hakimu Mkuu
Asanteni nyoter kwa ukarimu wenu usio kifani na
taasisi za ajabu ambazo mmejenga hapa Ghana.sAS
sasa, nazungumza nanyi baada ya ziara ndefu.
Nilianzia Russia, kwa mkutano wa mataifa mawili makubwa.
Nikasafiri kuelekea Italia, kwa mkutano wa mataifa yanayoongozaq katika uchumi duniani.
Na nimekuja hapa, Ghana, kwa sababu moja rahisi:
karne ya 21 itaathiriwa na kile kinachotokea si Roma peke yake
au Moscow au Washington, lakini na kile kinachotokea Accra vile vile.
(kushan gilia na makofi)
Huu ni ukweli mtupu wa wakati ambapo mipaka baina
ya watu inazidiwa nguvu na uhusiano wetu.
Ustawi wenu unaweza kupanua ustawi wa Marekani.
Afya yenu na usalama vinaweza kuchangia kwa afya ya dunia
na usalama.
And the strength of your democracy can help advance human Na uimara wa demokrasia yenu unaweza kusaidia kuendeleaza
rights for people everywhere. haki za binadamu kwa watu kila mahali.
Kwa hiyo sizioni nchi na watu wa Afrika kama ulimwengu
uliojitenga; naiona Afrika kama sehemu muhimu
ya ulimwegu wetu unaohusiana-- kama washirika wa Marekani kwa niaba ya
mustakabali tunaowatakia watoto wetu wote.
Ushirika huo lazima msingi wake uwe uwajibikaji wa
pande zote na kuheshimiana,
na hilo ndilo ninalotaka kulizungumzia leo.
Ni lazima tuanze na kanuni ya kimsingi kwamba mustakabali wa Afrika
ni uamuzi wa Waafrika wenyewe.
Nasema haya nikijua kabisa maafa yaliyopita ambayo wakati mwingine
yamedhuru sehemu hii ya dunia.
Baada ya yote, ninayo damu ya Afrika ndani yangu--
(kushangilia na makofi)
---na hadithi ya familia yangu imepitia yote maafa
na ushindi wa hadithi kamili ya Afrika.
Baadhi yenu mnajua, babu yangu alikuwa mpishi wa Waingereza
nchini Kenya, na ingawa alikuwa mzee anayeheshimika kijijini kwake,
waajiri wake walimwita "mvulana" kwa wakati mwingi wa maisha yake.
Alikuwa kwenye ukingo wa harakati za ukombozi wa Kenya
lakini bado alifungwa kwa muda wakati wa ukandamizaji.
Wakati wa maisha yake ukoloni haukuwa tu kuundwa kwa mipaka isiyo ya
asili au uonevu uliokuwepo katika biashara--
ni kitu ambacho kila mtu alipitia, siku baada ya siku
mwaka baada ya mwaka.
Baba yangu alikua akichunga mbuzi katika kijiji kidogo,
umbali usiopimika kutoka vyuo vikuu vya Marekani ambako
alikuja kupata elimu.
Alikomaa wakati wa enzi ya matumaini makubwa katika Afrika.
Harakati za kizazi cha baba yake yalikuwa yanazalisha
mataifa mapya, kuanzia hapa hapa Ghana.
(kushangilia na makofi)
Waafrika walikuwa wakipata elimu na kuonyesha uwezo wao katika njia mpya
na historia ilikuwa inabadilika.
Lakini licha ya maendeleo ambayo yamefanyika--
na kumekuwepo maendeleo makubwa katika maeneo mengi ya Afrika
--tunajua vile vile kwamba ahadi hiyo bado haijatimizwa.
Nchi kama Kenya ilikuwa na uchumi wa pato kubwa kwa kila mtu kuliko
Korea Kusini wakati nilipozaliwa.
Zimepitwa nyuma vibaya sana.
Maradhi na migogoro vimevuruga sehemu kadhaa za bara.
Katika maeneo mengi, matumaini ya kizazi cha baba yangu yamegeuka kuwa
mashaka, hata kukata tamaa.
Sasa, ni rahisi kunyoosha vidole na kubandika lawama hizi
kwa watu wengine.
Ndiyo, ramani ya ukoloni isiyoeleweka ilisaidia kuzalisha
migogoro; nchi za magharibi mara nyingi zimeitendea Afrika kama mlezi
na chanzo cha mapato badala ya mshirika.
Lakini nchi za magharibi haziwajibiki na kuharibiwa kwa
uchumi wa Zimbabwe katika mwongo uliopita,
au vita ambamo watoto wanaandikishwa kama wapiganaji.
Wakati wa uhai wa baba yangu, ulikuwa ni ukabila na ubaguzi
na upendeleo katika Kenya huru ambao kwa muda mrefu,
ulimvurugia kazi yake, na tunajua kwamba ufisadi wa aina hii
ni maisha ya kila siku kwa watu wengi sana.
Sasa, tunajua pia kuwa hiyo si hadithi nzima.
Hapa Ghana, mmetuonyesha uso wa Afrika ambayo mara
nyingi inapuuzwa na ulimwengu unaotizama maafa tu na mahitaji ya hisani.
Watu wa Ghana wamefanya kazi kwa bidii kuiweka demokrasia kwenye
msingi imara kukiwa na mabadiliko ya mara kwa mara ya utawala hata
katika uchaguzi ulioshindaniwa vikali.
(kushangilia na makofi)
Na kwa kuongezea, naomba nisema pia kwamba kwa hilo, walio wachache wanastahili
sifa nyingi kama walio wengi.
(kushangilia na makofi)
Na kukiwa na utawala bora ulioimarika na jamii ya kiraia,
uchumi wa Ghana umeonyesha kima cha kuvutia sana katika ustawi.
(kushangilia)
Maendeleo haya huenda yasiwe na msisimuko wa harakati za
ukombozi, Lakini msiwe na shaka: hatimaye yatakuwa muhimu zaidi.
Kwa kuwa ni muhimu kuibuka kutoka udhibiti wa
taifa jingine, ni muhimu zaidi kujenga taifa lenu wenyewe.
Kwa hiyo naamini kwamba muda huu ni muafaka kwa Ghana--
na kwa Afrika--kama muda ule ambapo baba yangu alikomaa na
mataifa mapya yakiwa yanazaliwa.
Huu ni muda mpya wa matumaini makubwa.
Tofauti pekee ni kwamba wakati huu tumejifunza kuwa haitakuwa watu mashuhuti kama
Nkrumah na Kenyatta ambao wataamua mustakabali wa Afrika.
Badala yake, itakuwa ninyi -- wanaume kwa wanawake katika
bunge la Ghana, watu mnaowakilisha.
Itakuwa ni vijana--wakijawa na vipawa na nguvu
na matumaini -- ambao wanaweza kudai mustakabali ambao kwa wengi katika
vizazi vilivyopita hawakuyafanikisha.
Sasa, kuweza kuitimiza ahadi hiyo, ni lazima kwanza tutambue
ukweli wa kimsingi ambao ninyi Ghana mmeupa uhai:
maendeleo hutegemea utawala bora.
(kushangilia)
Hicho ni kiungo ambacho kimekosekama katika
maeneo mengi sana, kwa muda mrefu.
Hayo ni mabadiliko ambayo yanaweza kufungua uwezo wa Afrika.
Na huo ni wajibu ambao unaweza kutimizwa tu na Waafrika.
Na kuhusu Marekani na nchi za magharibi, ahadi yetu lazima ipimwe
si kwa dola tu tunazotumia.
Nimeahidi mwongezeko mkubwa katika misaada yetu ya
kigeni, ambayo ni kwa maslahi ya Afrika na Marekani.
Lakini dalili halisi za ufanisi si kama sisi ni chanzo
misaada ya daima ambayo inawasaidia watu kusalimika--
ni kama sisi ni washirika katika kujenga uwezo
wa mabadiliko ya kimsingi.
9kushangilia na makofi)
Wajibu huu wa pande zote lazima uwe msingi wa ushirika wetu.
Na leo, nitamulika maeneo manne ambayo ni muhimu
kwa hali ya siku za mbele ya Afrika na ulimwengu mzima unaoendelea; demokrasia;
fursa; afya; na kutanzuliwa kwa migogoro kwa njia za amani.
Kwanza, ni lazima tuunge mkono serikali za demokrasia imara na endelevu
(kushangilia na makofi)
Kama nilivyosema mjini Cairo, kila taifa linaipa demokrasia uhai
katika njia zake za kipekee, na kwa kuzingatia jadi yake.
Lakini historia imetoa uamuzi bayana:
seriakali ambazo zinaheshimu utashi wa watu wao ambazo
zinatawala kwa ridhaa na si kulazimisha
ziko imara zaidi, na zinafanikiwa zaidi kuliko serikali zisizofanya hivyo.
Hii ni zaidi tu ya kufanya uchaguzi--
pia ni juu ya kile kinachotokea kati ya uchaguzi na uchaguzi
(kushangilia)
Unajua, ukandamizaji unaweza kuchukua mwundo mbalimbali,
na mataifa mengi--hata yale yanayofanya uchaguzi--
yanakabiliwa na matatizo ambayo husababisha watu wao kuwa mafukara.
Sasa, hakuna nchi ambayo itaunda utajiri kama viongozi wake
wanatumia uchumi kujitajirisha wenyewe--
(kushangilia na makofi)
--au kama polisi anaweza anaweza kununuliwa na wauzaji madawa ya kulevya.
Hakuna biashara inayotaka kuwekeza katika sehemu ambako serikali inajichukulia
asilimia 20% ya mtaji---
9kushangilia na makofi)
--au mkuu wa Mamlaka ya Forodha ni mla rushwa.
Hakuna mtu anayetaka kuishi katika jumuiya ambakop utawala wa kisheria
umegeuzwa kuwa utawala wa kikatili na hongo.
(kushangilia)
Hiyo si demokrasia, huo ni utawala wa kimabavu,
hata kama mara kwa mara utanyunyiziwa na uchaguzi wa hapa na pale.
Na sasa muda umewadia kwa mtindo huo wa utawala kukomeshwa.
Katika karne ya 21, taasisi zenye uwezo,
zinazoaminika, nas zilizo wazi ndio ufunguo wa mafanikio --
mabunge imara, majeshi ya polisi yaliyo waaminifu, mahakimu walio huru--
(kushangilia)
--vyombo vya habari vilivyo huru; na sekta ya kibinafsi iliyochamgamka;
jamii ya kiraia; hivyo ni vitu vinavyoipa demokrasia uhai,
kwa sababu ndivyo vitu vya maana katika maisha ya kila siku ya watu.
Sasa, mara kwa mara, Waghana wamechagua utawala wa kikatiba
juu ya utawala wa nguvu, na kuonyesha moyo ea kidemocrasia ambao unaruhusu
nguvu za watu wenu kufanikiwa.
(kushangilia)
Tumeiona hiyo katika viongozi wanakubali kushindwa kiungwana-- 00:13:17:533, 00:13:21:433 ukweli kwamba washindani wa Rais Mills walisimama
naye jana usiku kulisalimu niliposhuka kwenye ndege
inasema mengi juu ya Ghana.
(makofi)
washindi ambao hawatii miito ya kuwataka watumie nguvu dhidi ya
wapinzani kwa uonevu.
Tumeiona roho hiyo katika waandishi wa habari kama
Anas Aremayew Anas, ambaye alihatarisha uhai wake kuripoti ukweli.
Tumeiona katika polisi kama Patience Quaye,
aliyesaidia kuanzishwa mashtaka mwuzaji wa kwanza wa binadamu nchini Ghana.
Tumeiona katika vijana ambao wanalalamikia
upendeleo, na kushiriki katika mchakato wa kisiasa.
Kote Afrika, tumeshuhudia mifano isiyohesabika ya watu
wakidhibiti mustakabali wao wenyewe, na kufanya mabadiliko kuanzia
chini hadi juu.
Tumeiona nchini Kenya, ambako jumuiya ya kiraia na biashara
zilishirikiana kusimamisha machafuko yaliyotokea baada ya uchaguzi.
Tuliiona Afrika kusini, ambako zaidi ya robo tatu ya
nchi walishiriki katika uchaguzi wa hivi karibuni--
wa nne kufanyika tangu mwisho wa sera za ubaguzi wa rangi.
Tuliiona Zimbabwe, ambako kundi la Election Support Network lilikabiliana
kwa ujasiri na ukandamizaji kutetea kanuni kwamba
kura ya mtu ni haki yake isiyopingika.
Sasa, na wahakikishia: historia iko upande wa
Waafrika; si wale wanaotumia mapinduzi au kubadilisha katiba
kubaki madarakani.
(kushangilia na makofi)
Afrika haihitaji wababe, inahitaji taasisi imara.
(kushangilia)
Sasa, Marekani haina nia ya kulazimisha mfumo wowote wa serikali
kwa taifa jingine lolote.
Ukweli wa msingi wa demokrasia ni kwamba kila taifa linajiamulia
mwelekeo wake.
Lakini itakachofanya Marekani, ni kuongeza msaada kwa
watu na taasisi zinazowajibika ikimulika
kusaidia utawala bora--
katika mabunge ambayo yanadhibiti ubadhirifu wa mamlaka na kuhakikisha kwamba
sauti za upinzani zinasikika; utawala wa kisheria,
ambao unahakikisha utoaji sawa wa haki;
juu ya kushiriki kwa raia, ili vijana waweze kuhusika;
na ufumbuzi dhahiri wa ufisadi kama vile uwajibikaji kwa umma
na huduma zinazotolewa na mashini,
kuimarisha simu za kuripoti ubadhirifu, na kuwalinda wanaotoa siri za matumizi mabaya ya
madaraka ili kuendeleza uwazi na uwajibikaji.
Na tunatoa msaada huu, nimeamuru serikali yangu
kumulika zaidi rushwa katika ripoti yetu juu ya Haki za Binadamu.
Watu kila mahali wanapaswa kuwa na haki ya kuanzisha biashara au
kupata elimu bila kulipa hongo.
(kushangilia)
tuna wajibu wa kuwasaidia wale wanaochukua hatua za
kuwajibikia na kuwatenga wanaotenda kinyume,
na hivyo ndivyo Marekani itakavyofanya.
Sasa, hili linaelekeza moja kwa moja kwa eneo la oili la ushirikiano wetu--
kusaidia maendeleoyatakayotoa fursa kwa watu wengi zaidi.
kukiwa na utawala bora, sina shaka kwamba Afrika inayo
matumaini ya msingi mpana zaidi wa ustawi.
Shuhudia ufanisi wa ajabu wa Waafrika wengi nchini
mwangu, Marekani.
Wanafanya vizuri sana.
Kwa hiyo wana kipaji, wana roho ya ujasiriamali;
suali ni je, tutahakikishaje kwamba
wanafanikiwa katika nchi zao?
Bara lina utajiri wa maliasili.
Na kuanzia wajasiriamali wa simu za mkononi hadi wakulima wadogo,
Waafrika wameonyesha uwezo na moyo wa kujiundia
fursa zao wenyewe.
Lakini tabia za kale pia lazima zivunjwe.
Utegemeaji wa bidhaa---au zao moja linalouzwa nje--
una tabia ya kurundika utajiri mikononi mwa wachache,
na kuwaacha watu katika udhaifu wa kuathirika na uchumi unaodidimia.
Kwa hiyo nchini Ghana, kwa mfano,mafuta yameleta fursa kubwa,
na mmewajibika ipasavyo kujitayarisha kwa mapato mapya.
Lakini kama wajuavyo Waghana wengi, mafuta hayawezi kuwa kakao mpya.
Kuanzia Korea Kusini hadi Singapore, historia imeonyesha kwamba nchi zina
stawi kwa kuwekeza katika watu wake na katika
miundombinu; pale--
(kushangilia na makofi)
--pale wanapoendeleza viwanda vya bidhaa zinazouzwa nje
na kukuza kundi la wafanyikazi wenye ujuzi, na kuunda nafasi kwa biashara
ndogo na za kadiri zinazobuni ajira.
Na jinsi Waafrika wanavyoifikia ahadi hii,
Wamarekani watakuwa na wajibu zaidi kunyoosha mkono wetu.
Kwa kupunguza gharama zinazokwenda kwa washauri wa kimagharibi na
utawala, tunataka kuweka raslimali mikononi mwa
wale wanaohitaji, huku tukitoa mafunzo kwa watu kujitegemea zaidi
(makofi)
Hii ndiyo sababu hatua yetu ya dola bilioni 3.5 katika mpango wa usalama wa chakula
inamulika kubuni njia mpya na teknolojia kwa wakulima
si kuwapeleka tu wazalishaji wa Kimarekani au bidhaa barani Afrika.
Na msaada peke yake si ufumbuzi
Lengo la misaada ya kigeni lazima liwe
kuunda hali ambazo zitawezesha misaada hiyo kutohitajika tena.
Nataka kuwaona Waghana si wanajitosheleza tu katika chakula,
nataka kuona mnauza chakula nje kwa nchi nyingine na kujipatia fedha.
Mnaweza kufanya hivyo.
(makofi)
Sasa, Marekani inaweza pia kufanya zaidi kuhimiza biashara na uwekezaji.
Mataifa tajiri lazima yafungue milango yetu kwa bidhaa na huduma
kutoka Afrika kwa njia ya maana.
Na hiyo ndiyo ahadi ya serikali yangu.
Na pale ambapo kuna utawala bora,
tunaweza kupanua ustawi kupitia ushirikiano wa raia na makundi ya kibinafsi
ambao unawekeza katika barabara nzuri na umeme;
kujenga uwezo kwa kutoa mafunzo kwa watu waanzishe biashara zao;
na huduma za kifedha ambazo zitawafikia si wakazi wa mijini tu,
bali pia mafukara katika maeneo ya mashambani.
Hili pia ni kwa ajili ya maslahi yetu—
kwa kuwa watu wanaponyanyuliwa kutoka kwenye ufukara na utajiri kuundwa
Afrika, unajua nini?
Masoko mapya yatafunguka kwa bidhaa zetu.
Kwa hiyo ni manufaa kwa wote.
Eneo moja ambalo linaonekana kuwa la hatari zisizosutwa
na lenye matumaini yasiyo na kifani ni nishati.
Afrika hutoa kiasi kidogo cha hewa chafu kulinganishwa na sehemu nyinginezo duniani,
lakini ni bara linalotishiwa zaidi na mabadiliko ya hali ya hewa.
Sayari inayozidi kuongezeka joto itasambaza maradhi, kupunguza fungu la maji
na kutokomeza mimea, na kuunda hali ambazo huleta
baa la njaa zaidi na migogoro.
Sisi wote—hasa ulimwengu ulioendelea— 00:20:24.834, 00:20:27.900 tunao wajibu wa kupunguza kasi ya mielekeo hii—
kupitia hatua za kuzuia na kubadilisha njia tunazotumia nishati.
Lakini tunaweza pia kushirikiana na Waafrika kugeuza mgogoro huu kuwa
fursa ya manufaa.
Kwa pamoja, tunaweza kushirikiana kwa niaba ya sayari yetu na
ustawi, na kuzisaidia nchi kuongeza uwezo wa kupata nishati—
bila kupitia katika awamu chafu ya maendeleo.
Hebu fikiria: Kote barani Afrika, kuna wingi wa nishati ya upepo
na jua; joto la ardhi na nishati inayotokana na viumbe.
Kuanzia Rift Valley hadi jangwa la Kaskazini;
kuanzia mwambao wa magharibi hadi mimea ya Afrika kusini—
maliasili za Afrika zisizo na kikomo zinaweza kuzalisha nishati yake zenyewe,
na kuuza nje kwa faida nishati iliyo safi.
Hatua hizi si juu ya takwim za ustawi tu kwenye orodha.
Ni juu ya kama kijana aliye na elimu anaweza kupata
kazi ya kipato kitakachomwezesha kutunza familia yake; mkulima anaweza kusafirisha bidhaa zake .
sokoni; au mjasiriamali mwenye wazo la kibunifu anaweza kuanzisha biashara yake.
Ni juu ya heshima ya kuwa na kazi;
ni juu ya fursa ambayo lazima iwepo kwa Waafrika
katika karne ya 21.
Kama vile utawala bora ulivyo muhimu kwa fursa,
ni muhimu vile vile kwa eneo la tatu ambalo nataka kuzungumzia—
kuimarisha afya ya umma.
Katika miaka ya karibuni, maendeleo makubwa yamefanyika katika sehemu kadhaa
za Afrika.
Watu wengi zaidi wanaishi vizuri wakiwa na ***/AIDS,
na kupata dawa wanazohitaji.
Nimeona zahanati na hospitali nzuri inayomulika zaidi
afya ya akina mama.
Lakini wengi sana bado wanaendelea kufa kutokana na magonjwa ambayo hayapaswi kuua.
Watoto wanapouawa kwa kuumwa na mbu,
na akina mama wanaokufa wakati wa kujifungua
hapo ndipo tunapotambua kuwa lazima maendeleo yafanyike.
Lakini kutokana na vishawishi—mara nyingi vikitolewa na mataifa wafadhili,
madaktari wengi sana na manesi wa Afrika wanakwenda nchi za ng’ambo,
au hufanyia kazi programu zinazopambana na gonjwa moja tu.
Hii inaunda pengo katika huduma za msingi na uzuiaji.
Wakati huo huo, Waafrika binafsi lazima wafanye maamuzi ya kuwajibika mma katika jumuiya na nchi zao.
katika kuzuia kuenea kwa magonjwa,
wakati huo huo wakihimiza afya ya umma katika jumuiya na nchi zao.
Kwa hiyo kote barani Afrika, tumeona mifano ya watu wakitatua
matatizo haya.
Nchini Nigeria, juhudi zinazoshirikisha imani mbalimbali baina ya Wakristo na Waislamu
zimeweka mfano wa ushirikiano katika kupambana na malaria.
Hapa nchini Ghana na kote barani Afrika, tumeona mawazo ya ubunifu
yakijaza pengo katika huduma za matunzo—kwa mfano,
kupitia mipango kama E-Health Initiatives ambayo imewawezesha madaktari katika miji mikuu
kuwasaidia wale wanaofanya kazi katika miji midogo.
Marekani itaunga mkono juhudi hizi kupitia mkakati kamili
wa afya ya kimataifa.
Kwa sababu katika karne ya 21, tunatakiwa kuchukua hatua
na dhamira yetu na maslahi yetu ya pamoja.
Kwa sababu mtoto anapofariki kutokana na ugonjwa unaozuilika mjini Accra,
hiyo inatupunguzia sote kila mahali.
Na magonjwa yanapoenea bila kudhibitiwa katika pembe yoyote ya ulimwengu huu,
tunajua kwamba yanaweza kusambaa kuvuka mabahari na mabara.
Hii ndiyo sababu serikali yangu imeahidi kutoka dola billioni 63
kukabiliana na changamoto hizi.
dola billioni 63
(makofi)
Tukiendeleza juhudi imara zilizoanzishwa na Rais Bush,
tutaendeleza mapambano dhidi ya ukimwi, ***/AIDS.
Tutaendelea kulisaka lengo la kutokomeza vifo kutokana na malaria
na kifua kikuu, na kutokomeza polio.
(makofi)
Tutapambana na maradhi yaliyopuuzwa ya nchi za tropiki.
Na hatutakabiliana na maradhi haya kwa kujitenga—
tutawekeza katika mifumo ya afya za jamii ambayo inaweza kuzuia maradhi na kuhimiza uzima,
na kumulika afya ya akina mama na watoto.
(makofi)
Sasa,jinsi tunavyoshirikiana kwa ajili ya hali ya siku za mbele yenye afya,
ni lazima pia tusimamishe madhara yanayotokana na si maradhi tu,
lakini binadamu—
na eneo la mwisho nitakalozungumzia ni migogoro.
Sasa nitakuwa wazi kabisa: Afrika si ile picha ya katuni inayoonyesha
bara lililokumbwa na vita vya daima.
Lakini tukiwa wawazi, kwa Waafrika wengi,
migogoro imekuwa sehemu ya maisha, ikidumu kama vile jua.
Kuna vita ya kugombea ardhi na vita vya kugombea mapato.
Na bado ni rahisi sana kwa wale wasio na dhamira
kuchochea jamii nzima kupigana baina ya imani na makabila.
Migogoro hii ni kama mnyororo kwenye shingo ya Waafrika.
Sote tuna hulka nyingi—
za kikabila; dini na utaifa.
Lakini kujiona mwenyewe kwa
kupingana na mtu anayetoka kabila tofauti, au anayeabudu mtume
tofauti hakuna nafasi katika karne ya 21.
(kushangilia na makofi)
Tofauti za makabila Afrika zinapaswa kuwa chanzo cha nguvu, n
na si sababu ya mfarakano. na kupata fursa; kupenda ndugu na jamaa zetu, jumuiya zetu, na imani zetu. Huo ndio ubinadamu wetu.
Sisi sote ni watoto wa Mwenyezi Mungu.
Sote tuna mahitaji yanayofanana—
kuishi kwa amani na usalama; kupata elimu na
fursa; kupenda familia zetu na jumuiya,
na imani zetu.
Huo ndio ubinadamu wetu.
Hii ndiyo sababu lazima sote tusimame pamoja kupinga unyama katikati yetu.
Kamwe hakuna sabababu—hakuna sababu ya kuwalenga wasio na hatia
katika jina la itikadi.
Ni adhabu ya kifo kwa jumuiyainayowalazimisha watoto
kuua katika vita.
Ni kilele cha unyama na uhalifu
kuwaweka wanawake katika vitendo vya mfumo wa kubakwa bila kikomo.
Ni lazima tuwe mashahidi kwa thamani ya kila mtoto katika Darfur
na heshima ya kila mwanamke nchini Congo.
Hakuna imani au utamaduni unaopaswa kuhalalisha mabaya wanayotendewa.
Sisi sote kwa pamoja lazima tujitahidi kutafuta amani na usalama unaohitajika
kwa ajili ya maendeleo.
Waafrika wamesimama kidete kutetea hali hii ya siku za mbele.
Hapa pia, Ghana inasaidia kuelekeza njia inayofaa.
Waghana wanapaswa kuwa na fahari kwa mchango wenu katika juhudi za ulinzi wa amani
katika juhudi za ulinzi wa amani kuanzia Congo hadiLiberia na Lebanon
(makofi)
--na katika juhudi zenu za kupambana na baa la madawa ya kulevya.
(kushangilia na makofi)
Tunafurahia juhudi zinazochukuliwa na mashirika kama vile Umoja wa Afrika
na ECOWAS kufumbua migogoro, .
kulinda amani na kuwasaidia wale walio na shida
Na tunashawishi mtazamo wa mwundo wa chombo imara,
cha ulinzi katika eneo kinachoweza
kushirikisha majeshi ya mataifa mbalimbali wakati yatakapohitajika.
Marekani inao wajibu wakushirikiana nanyi,
kuendeleza mtazamo huu, si kwa maneno tu,
lakini kwa msaada unaoweza kuimarisha uwezo wa nchi za Kiafrika
Kunapotokea mauaji ya kimbari katika Darfur au magaidi Somalia,
haya si matatizo ya Afrika peke yake--
ni changamoto ya kimataifa katika ulinzi,
na yanahitaji mwitikio wa kimataifa.
Ndiyo maana tuko tayari kuwa washirika kupitia diplomasia, . (Makofi
misaada ya kitaalamu na misaada ya upangaji na uchukuzi,
na tutaunga mkono juhudi za kuwawajibisha wahalifu wa kivita.
Na nitasema wazi: Kamandi yetu ya Afrika inamulika
si kuanzisha vituo barani Afrika,
lakini katika kupambana na changamoto hizi za pamoja ili kuendeleza
usalama wa Marekani, Afrika na ulimwengu.
(kushangilia na makofi)
Mjini Moscow nilizungumzia haja ya kuwepo mfumo wa kimataifa
ambako haki za binadamu duniani zinaheshimika,
na ukiukwaji wa haki hizo unapingwa
Hiyo lazima ijumuishe ahadi ya kuunga mkono wale wanaoamua
kufumbua migogoro kwa amani,na kuwasimamisha wale wasiounga,
don't, and to help those who have suffered. na kuwasaidia wale waliodhurika.
Lakini hatimaye, itakuwa ni demokrasia iliyostawi
kama ilivyo nchini Botswana na Ghana ambayo inaweza kurudisha nyuma sababu za migogoro,
na kuendeleza mipaka ya amani na ustawi.
Kama nilivyosema awali, hali ya siku za mbele ya Afrika ni uamuzi wa Waafrika wenyewe.
Watu wa Afrika wako tayari kujinyakulia mustakabali wao. , .
Na katika nchi yangu, Wamarekani wenye asili ya Kiafrika
—wakiwemo wengi waliohamia karibuni
wamestawi katika kila sekta ya jamii.
Tumefanya hivyo licha ya hali ngumu ya zamani,
na tumepata nguvu kutoka kwa urithi wetu wa Kiafrika.
Wakiwa na taasisi imara na nia ya dhati,
najua kwamba Waafrika wanaweza kutimiza ndoto zao mjini Nairobi na
Lagos; mjini Kigali na Kinshasa; mjini Harare na hapa hapa Accra.
(kushangilia na makofi)
Mnajua, miaka hamsini na mbili iliyopita, macho ya ulimwengu yaliimulika Ghana.
Na kasisi mmoja kijana aliyeitwa Martin Luther King, alisafiri
kuja hapa Accra, kushuhudia bendera ya Union Jack ikiteremshwa
na bendera ya Ghana ikipanda kwenye Bunge.
Hii ilikuwa kabla ya maandamano ya Washington au ufanisi wa
harakati za kupigania haki za kiraia katika nchi yangu.
Dakta King aliulizwa mjini Accra jinsi alivyojisikia kushuhudia kuzaliwa
kwa taifa.
Na akasema “Inafufua upya imani yangu katika
kushinda hatimaye kwa haki.”
Sasa, ushindi huo lazima upatikane mara nyingine tena,
na ni lazima upatikane kutokana nanyi
(kushangilia na makofi)
Na hapa nazungumza hasa kwenu vijana kote
Afrika na hapa Ghana.
Katika maeneo kama Ghana, vijana mko zaidi ya nusu ya idadi ya watu
Na hiki ndicho mnachopaswa kujua: ulimwengu ni kile mnachotaka kiwe. 00:31:12.900,00:31:15.800 Mnao uwezo wa kuwawajibisha viongozi wenu
na kujenga asasi ambazo zitahudumia watu.
Mnaweza kuhudumia jumuiya zenu,
kutumia nguvu zenu na elimu kuunda utajiri mpya
na kujenga uhusiano mpya na dunia.
Mnaweza kuyashinda maradhi,na kumaliza migogoro,
na kufanya mabadiliko kuanzia chini kwenda juu.
Mnaweza kufanya hivyo.
Ndiyo mnaweza
(kushangilia)
Kwa sababu wakati huu, historia inasonga mbele.
Lakini vitu hivi vinaweza kufanyika tu kama wote mtachukua
wajibu wa hali zenu za baadaye.
Na haitakuwa rahisi.
Itachukua muda na juhudi.
Kutakuwepo maumivu na pingamizi.
Lakini naweza kuwaahidi hili: Marekani itakuwa nanyi katika
kila hatua.
Kama mshirika.
Kama rafiki.
(kushangilia na makofi)
Fursa haitatokea kutoka eneo jingine lolote--
Lazima itokane na maamuzi mnayoyafanya,
na vitu mnavyofanya,matumaini mliyo nayo mioyoni mwenu
Ghana,uhuru ni urithi wenu.
Sasa, ni wajibu wenu kujenga juu ya msingi wa uhuru huo,
Na kama mtafanya hivyo, miaka ya baadaye tutatizama tena mahali kama
hapa Accra na kusema huu ulikuwa wakati ambapo ahadi ilitimia--
huu ndio wakati ambapo ustawi ulibuniwa;
tulivuka maumivu, na enzi mpya ya maendeleo ilianza
Huu unaweza kuwa wakati ambapo tunashuhudia ushindi wa haki kwa mara nyingine tena
Ndiyo tunaweza.
Asante sana.
Mungu awabariki.
Asante.
(kushangilia na makofi) �