Tip:
Highlight text to annotate it
X
Linganisha na nabii za wazi kuhusu Yesu katika Biblia.
Kwahiyo tumeona hizi nabii zinazosemekana za Muhammad katika Biblia,
na tunapozilinganisha
na nabii kuhusu kuja kwa Yesu,
ni kama mchana na usiku.
Nabii za kuja kwa Yesu ziko wazi kabisa,
kiasi kwamba hakuna swali
kuhusu kile kilichosemwa.
Hebu tuangalie kwa mfano katika Isaiah 53,
hebu soma mistari tu.
Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta?
Na mkono wa Bwana
amefunuliwa nani?
Hakika ameyachukua masikitiko yetu
Amejitwika huzuni zetu,
Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa na Mungu
Amepigwa , na kuteswa.
Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu,
Alichubuliwa kwa maovu yetu;
Adhabu ya amani yetu
ilikuwa juu yake, na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
Sisi sote kama kondoo tumepotea;
Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe;
Na Bwana ameweka juu yake
Maovu yetu sisi sote.
Alionewa, lakini alinyenyekea,
wala hakufunua kinywa chake;
alikuwa kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni,
Na kama vile kondoo anyamazavyo mbele yao wakatao manyoya yake;
Naam, hakufunua kinywa chake.
Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa.
Na maisha yake ni nani atakayeisimulia?
Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai;
Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya;
Na pamoja na matajiri katika kufa kwake;
Ingawa hakutenda jeuri,
Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
Lakini Bwana aliridhika kumchubua
Amemhuzunisha;
Bwana takapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi
Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi,
Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake.
Baada ya taabu ya nafsi yake,
Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika
Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki
Atawafanya wengi kuwa wenye haki;
Naye atayachukua maovu yao.
Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu,
Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari;
Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa
Akahesabiwa pamoja na hao wakosao.
Walakini alichukua dhambi za watu wengi,
Na kuwaombea wakosaji.
Kwahiyo tunaweza kuona kwa uwazi kwamba hiyo inaongelea kuhusu mtu
ambaye amelaaniwa kwa ajili ya walio wengi,
ni nani angechukua dhambi mabegani mwake,
ni nani angeteseka,
na ni nani angekataliwa na kudharauliwa na watu.
Huu ni unabii wa wazi kabisa
kuhusu kuja kwa Yesu.
Na inaongea juu ya kuja kwa mtu.
Linganisha huo na nabii mbalimbali
kuhusu Muhammad katika Biblia,
ambazo kimsingi siyo nabii.
Unasema kwamba 'atakwenda kuwa ''jamaa''
ya Waisraeli,
lakini Muhammad hakuwa.
Katika Isaya, ambao ni ''unabii'',
unaodaiwa kuwa unabii,
wala hauogelei kuhusu kuja kwa mtu.
na vivyo hivyo kwa Wimbo Ulio Bora.
Na katika kitabu cha Yohana,
tunaongea kuhusu Roho Mtakatifu.
wakati hapa unabii unasema wazi wazi kuhusu mtu
atakaye teseka kwa ajili ya maovu yetu
na kuchukua dhambi zetu.
Unazungumza kuhusu Yesu
kwa uwazi kabisa.
Kuna tofauti kubwa kati ya
nabii kuhusu Yesu katika Biblia
na zinazodaiwa kuwa''nabii'' kuhusu Muhammad.