Tip:
Highlight text to annotate it
X
Wapendwa ndugu zangu waume kwa wake,
Kwa moyo wa dhati na shukurani , nawatakieni nyote Baraka za Pasaka, kwa kumnukuu Mtakatifu Augustine, Resurretio Domin Spes Nostra, Ufufuko wa Bwana wa Tumaini letu.
Kwa maneno haya , Askofu Mshuhuri aliwaeleza Waamini Kwamba, Yesu alifufuka tena, ili kwamba, sisi, ingawa hatima yetu ni kifo ,tusikate tamaa na kuwa na hofu kwamba , kwa kifo maisha yanamalizika kabisa.
Yesu amefufuka ili tupate tumaini.
Katika ukweli wake, kati ya masuala yenye kuwatatiza sana wake kwa waume ni hili, kuna nini baada ya kifo,
Katika fumbo hili ,adhimisho la leo linaruhusu kutoa jibu kwamba, kifo si neno la mwisho , kwa sababu maisha hupata ushindi mwishoni.
Uhakika huu wetu, misingi yake si tu kwa hoja nyepesi za binadamu , lakini ni ukweli wa imani katika historia.
Yesu Kristu , aliyesulubiwa na kuzikwa , amefufuka kwa utukufu
Yesu amefufuka ili sisi pia , kwa kumwamini yeye , tuweze kuwa na uzima wa milele.
Mbiu hii ndiyo kiini cha ujumbe wa Injili , kama Mtakatifu Paulo alivyotangaza kwa nguvu
kama Kristu hakufufuka , kuhubiri kwetu ni bure na imani yetu ni bure.
Anaendelea kusema,: kama katika maisha haya tunaweka tumaini letu katika Krsitu tunakuwa watu wa kuhurumiwa kuliko wote.
Tangu mapambazuko ya Pasaka , chemichemi mpya ya tumaini imeijaza nchi ; kutokea siku hii na kuendelea ufufuko wetu ulianza , kwa sababu Pasaka haimaanishi kuwa ishara ya kawaida ya wakati wa kihistoria , lakini ni mwanzo wa hali mpya.
Yesu alifufuka si ili kumbukumbu yake ibaki katika mioyo ya wafuasi wake , lakini kwa sababu yeye mwenyewe anaishi ndani mwetu , na katika Yeye tayari tumekombolewa kwa furaha ya uzima wa milele.
Ufufuko hivyo si nadharia , lakini ni ukweli wa historia iliyofunuliwa na Mungu Mtu, Yesu Kristu kwa njia ya mateso na kifo,
kiichofungua njia mpya kati ya mbingu na dunia (cf Heb10:20)
si hadithi, wala ndoto , si maono au kufikirika , si riwaya, lakini ni tukio la kipekee na lisilo jirudia:
Yesu Kristu wa Nazareth , Mwana wa Maria , ambaye katika machweo ya Ijumaa , alishushwa msalabani na kuzikwa, kwa ushindi mkuu aliondoka kaburini.
Ni kweli katika mapambazuko ya siku ya kwanza, baada ya Sabato , Petro na Yohana, walikuta kaburi wazi.
Maria Magdalena , na wanawake wengine , walikutana na Yesu Mfufuka. Katika njia ya Damascus , wafuasi wake wawili walimtambua katika kuumenga mkate.
Aliyefufka anajionyesha kwa mitume wake jioni hiyo katika chumba cha Juu , na kwa wafuasi wengine wa Galileya.
Kutangazwa kwa Bwana Mfufuka , kuna mulika maeneo yenye giza katika dunia hii tunayoishi.
Ninarejea hasa moyo wa watu kupenda mali na ukana Mungu , katika mtazamo wa dunia isiyoweza kusonga mbele zaidi katika kile kilichokwisha thibitishwa kisayansi,
na kunywea bila furaha katika maana ya utupu unaofikiriwa kuwa ni hatima ya mwisho ya maisha ya binadamu.
Ni kweli kamba, kama Kristu hakufufuka , utupu unakuwa katika hali ya kudumu
kama tunamweka mbali Kristu na ufufuko wake , hakuna namna mtu anavyoweza kujinusuru , na kila mmoja tumaini lake linakuwa ni njozi.
Lakini leo hii, ni siku ambayo kutangazwa kwa ufufuko wa Bwana , kunafanyika kwa nguvu na ni jibu katika swali linalojitokeza mara kwa mara , juu ya shuku tunazozipata katika kitabu cha Mhubiri .
Je kuna kitu kilichoelezwa , angalia hiki ni kipya, (Ecc.1:10)
Tunajibu , ndiyo :kila kitu kilifanywa upya .
Kifo na Maisha kinapambana uso kwa uso: Bwana wa maisha alikufa , lakini sasa anaishi kwa ushindi mkuu .
Huu ndio upya? Upya wenye kubadili maisha ya wale wanaomkubali , kama ilivyo kwa Watakatifu
kwa mfano, ni kile kilichotokea kwa Mtakatifu Paulo .
Mara nyingi , kwa mtazamo wa mwaka wa Paulo, tumekuwa tukitafakari juu ya uzoefu wa Mtume huyu mashuhuri .
Saulo wa Tarsus, aliyekuwa mdhulumaji mkubwa Wakristu, alikutana na Yesu Mfufuka katika njia ya Damascus na kutekwa nae.
Menigne yaliyobaki tunayajua. Kwa Paulo kulitokea , kile baadaye alichokiandika juu yake kwa Wakristu wa Koritho.
Kwa anayekuwa ndani ya Kristu anakuwa kiumbe kipya: ya kale yamepita, tazama , upya unakuja (2Cor 5;17)
Na tutazame zaidi juu ya Mwinjilishaji huyu mashuhuri , ambaye kwa ushupavu, shauku kubwa , na mhemko wa kitume, aliipeleka Injili kwa watu mbambali katika dunia ya wakati ule.
Mafundisho yake na yawe mfano wenye kutuvuvia nasi kwenda kumpeleka Bwana Yesu kwa watu .
Na utuhimize sisi kumwamini Yeye , kwa sababu kwamba, maana ya utupu , ambao unamwelekeo wa kumsonga binadamu , umeshindwa, na Mwanga wa Tumaini, lile linalozuka kutoka katika Ufufuko.
Maneno ya Mzaburi , kweli ilitimizwa, giza si giza tena , usiku umekuwa mwanga kama siku (Ps 139(138):12)
Si utupu tena unaozingira vitu vyote , lakini upendo wa uwepo wa Mungu .
Ufalme huu wa kifo umewekwa huru , kwa sababu Neno la Uhai , limepita hata dunia ya kuzimu , kupitia uvuvio wa Roho(v8)
kweli kwamba , kifo hakina tena nguvu dhidi ya binadamu , na dhidi ya dunia, lakini bado kumebaki mengi, dalili nyingi za uweza wake wa nyuma,
hata kama kupitia Pasaka Kristu ameharibu mizizi yote ya uovu, bado anahitaji msaada wa wake kwa waume wa kila nyakati na mahali kumsaidia kuthitibisha ushindi wake kwa kutumia silaha zake : 46. silaha ya haki na ukweli, huruma msamaha na upendo.
silaha ya haki na ukweli, huruma msamaha na upendo.
Huu ni ujumbe ambamo wakati wa ziara yangu ya Kitume Cameroon na Angola,
nilipenda kuutoa kwa bara lote la Afrika ambako nilipokelewa kwa moyo wa dhati, shauku kuu na utayari wa kusikiliza.
Afrika inateswa na ukosefu wa uwiano, kutokana na ukatili na mizozo isiyokuwa na mwisho , mara nyingi iliyosahaulika, ikisababisha umwagaji wa damu mwingi na uharibifu katika baadhi ya mataifa yake,
na kutotkana na ongezeko la watu wake , waume kwa wake, anakuwa chambo cha njaa , ufukara na maradhi.
Nitarudia ujumbe huo ka nguvu zaidi , nitakapokuwa Nchi Taktifu , ambako nitafurahi kupatembelea katika muda wa wiki chache tokea sasa.
Mapatano ni jambo ngumu lakini linawezekana , na ni sharti la awali, kwa ajili ya ujenzi wa siku za baadaye zenye kuwa na uhakika wa usalama kwa ujumla na uwepo wa amani kwa ajil ya wote.
Na inawezekana tu kufanikisha kupitia juhudi mpya, udumishaji na uaminifu kwenye taratibu zinazolenga kutatua mgogogro kati ya Israel na Palestina.
Mawazo yangu sasa yanaondoka Nchi Takatifu hadi mataifa jirani ya Mashariki ya Kati , na dunia kwa ujumla.
katika nyakati za upungufu wa chakula , kipeo cha uchumi , mifumo ya kale na mipya ya ufukara na usumbufu unaoletwa na mabadiliko ya hali ya hewa,
ghasia na unyanyasaji unaolazimisha wengi kuteelekeza makazi yao na kutafuta sehemu zingine pa usalama zaidi kuishi ,
katika wakati huu, kitisho cha ughaidi, na kukua kwa hofu kwa siku za usoni,
inakuwa ni hoja ya kidharura, kungudua misingi ya tumaini.
Mtu yeyote na asirudi nyuma katika mapambano haya yaliyoanzishwa na Kristu Mfufuka.
Kama nilivyosema awali , Kristu anatafuta waume kwa wake wenye kupenda kumsaidia kuthibitisha ushindi wake kwa kutumia silaha zake mwenyewe,
silaha ya haki na ukweli, huruma , msamaha na upendo.
Resurretio Domin Spes Nostra! Ufufko wa Kristu Tumaini letu.
Kanisa leo hii linatangaza kwa furaha . Linatamka tumaini ambalo sasa ni thabiti na liloonekana kwa sababu Mungu amemfufua Kristu katika wafu,
analifikisha tumaini lake la dhati analolibeba katika mtima wake akipenda kuwashirikisha watu wote kila mahali,
hasa ambako wakristu wanateswa kwa sababu ya imani yao na uwajibikaji wao katika kutaka haki na amani,
linatoa wito wa tumaini ambao unaweza kuhimiza ushupavu wa kutenda mema hata kama itagharimu.
Leo Kanisa linaimba, hii ndiyo siku aliyoitengeneza Bwana , na kuwataka wote wafurahi .
Leo hii Kanisa linatoa wito wa sala kwa Mama Maria , nyota ya tumaini , likimwomba awaongoze binadamu, katika njia salama ya wokovu wa uwingu, ndani ya Moyo wa Kristu.
Dhabihu wa Pasaka, Mwana kondoo aliyeukomboa ulimwengu , asiyekuwa na hatia, aliyetupatanisha sisi wadhambi na Baba,
Kwake yeye Mfalme wetu mshindi , aliyesulubiwa na kufufuka , tunaimba kwa furaha Alleluia!