Tip:
Highlight text to annotate it
X
Watu wengi wanachukua maisha yao kila siku kwa sababu hili ni mwiko.
Biblia ni kitabu chenye hatari.
Katika FPO [Austrian populist party] walisema kuwa ushoga ni utamaduni wa kifo.
Kama haiwezekani kuachia kidogo utamaduni ili kuwapa vijana hisia ya.
kwamba wanaishi katika mazingira yasiyowatishia na kwa hiyo wanaweza kutochukua maisha yao,
basi huwezi kuongelea kuhusu kumpenda jirani yako
Biblia ni kitabu hatari. Kuna sehemu kadhaa zinazochangia watu kuwa dhidi ya mashoga.
Kuna sehemu moja, kwa mfano, inayosema kuwa kama wanaume wawili wakilala pamoja, basi wote lazima wauliwe.
Hasa inasema, “damu yao iwe juu yao”. Hii ni katika Mambo ya Walawi. Na pia iko kwenye Torati.
Katika Qu’rani haisemi kuwa wauliwe, bali waadhibiwe.
Kuna watu vichaa na mafanatiki kila mahali. Uwezekano wa mtu kufungua vitabu hivyo na kuua mtu
upo na utaendelea kuwepo, maadam vitabu hivi vitaendelea kubarikiwa kama neno la Mungu.
Kuna wachungaji ambao wanaokubaliana na ndoa za watu wa jinsia moja.
lakini kila mmoja anasoma kile anachotaka na anafafanua kile kinachomfaa yeye.
Ninafikiri ushoga ni kinyume cha sheria katika nchi 71 na kati ya hizi nchi, nane zina adhabu ya kifo kwa mashoga.
Ukubali wa ushoga ni mdogo kama asilimia mbili katika baadhi nchi
India kuna mahekalu ambapo unaweza kuona michoro ya watu wa jinsia moja wakifanya mapenzi, na pia watu wa jinsia tofauti.
Japan na China pia ilikuwa kama hivyo, unaweza kuthamini mambo haya katika sanaa, na fasihi
Peru na Ecuador kuna vijana wasagaji ambao wamewekwa katika kliniki maalum ambapo wanabakwa kwa sababu wazazi wao hawajui nini cha kufanya nao,
Askofu mkuu wa Oaxaxa, Mexico alisema muda mfupi uliopita kwamba hakuna mwanamke ama mwanaume msafi na mkweli ambaye atataka kuwa shoga.
Wengine wameongea dhidi ya haki za mashoga kuwa waalimu.
Mwaka jana kati ya makuhani 800 na 1000; Sijui kama ni marekani pekee ama dunia nzima kwa ujumla.
walisema kuwa ushoga ni wa kulaumiwa kwa tetemeko la ardhi la Haiti.
Berlusconi alisema, kwa mfano, kwamba ni bora kuwatendea wanawake kama afanyavyo
kuliko kuwa shoga, hata kama analala na wasichana wadogo!
Sio tu wanasiasa wa mrengo wa kulia wanaoongea hivi, bali kuna wa mrengo wa kushoto kama
Evo Morales wa Bolivia aliyesema sababu ya kuwa na mashoga wengi Ulaya;
ambayo ni upuuzi kwa sababu Bolivia kuna mashoga wengi kama Ulaya na
ni kwamba tu wanajificha zaidi kwa sababu hawawezi kuwa huru,
hasa kwa sababu ya watu kama yeye (Evo) ambaye anachangia mawazo ya kibaguzi
Alisema kuwa sababu kuna mashoga wengi Ulaya ni chakula ambacho kimebadilishwa kiini
Wakati ndoa za watu wa jinsia moja zilipohalalishwa mwaka jana Argentina, Askofu mkuu wa Buenos Aires
Alisema ilikuwa vitu ya Mungu. Na bila shaka alipata msaada kutoka kwenye Biblia kwa hilo.
Wanasema sio kawaida na pia ni kitu kisicho halisia, lakini hawaelewi kuwa ushoga
umeonekana kwa undani katika spishi 500 na imeorodheshwa katika 1500.
Hatuko tofauti kutoka na wanyama wengine. Ushoga umeonekana hasa hasa katika wanyama werevu,
kwa mfano, baina ya nyani.
Kulikuwa hakuna tabia za kibaguzi za mashoga zilizopatikana kwenye wanyama.
Tatizo ni kwamba shuleni wanaongea sana kuhusu ubaguzi wa rangi, kuhusu kukubali makundi ya watu tofauti,
lakini hawaongei kabisa kuhusu ubaguzi wa mashoga. Huwa wanaliacha hili.
Mara nyngi maneno ya kutukana na kukejeliana mashuleni, kama usemavyo umoja wa walimu wa Ujerumani, ni “shoga” ama “msenge”.
Walimu hawaingilii kati na wengi wao wanakubaliana na tabia hii.
Samahani, unaweza kufanya hivyo nyumbani? Inatia kinyaa.
Tutafanya utani. Uko tayari? Na wanasema “ndio bila shaka”.
Kwa vijana wengi sio rahisi maana inachukua muda mpaka ukubali, maana inakataliwa katika jamii.
Watoto hawana uhusiano na mashoga, ama hawajui kwamba wanao uhusiano,
na hii ndo maana kiwango cha vijana mashoga wanaojiua ni kikubwa kuliko cha vijana wa kawaida wanaojiua.
Hii ndo maana ni hatari sana kutumia neno “shoga” kama jambo baya.
Pia wasagaji vijana wanateseka sana kwa sababu hii.
Kanisa huongea dhidi ya ndoa za watu wa jinsia moja na kusema ndoa ni kwa sababu ya kuzaliana.
Hii haina maana sana sababu kwatu wengine ambao hawawezi kuzaa wanaruhusiwa kuoana.
Wanawake wa miaka 50, kwa mfano, wanaweza kuolewa na hakuna mtu anaichukulia hii kama skendo.
Na ni kwa sababu ya huu utamaduni mashoga hawajiamini
na hawaongelei haki zao hadharani.
na kwa bahati mbaya watu wenye kuguswa ndio wanaoongelea.
Hii ilikuwa ni sawa kwa watu weusi Marekani. Walikuwa ni watu weusi waliopigana dhidi ya ubaguzi.
Kwa upande wa mashoga ni sawa sawa, lakini sikubaliani na jinsi wanavyoliongelea.
Ni mara moja tu kwa mwaka kuna ‘parade’, katika miji ulimwenguni, hili kwangu halina maana.
Huwafanya watu kuthibitisha ubaguzi wao.
Nadhani wengi wanafanya hivi kwa kukejeli. Wanaonesha tabia ambazo jamii inatuhusisha nazo.
Na unajicheka. Lakini watu wengi hawaelewi na wanafikiri mashoga
ni watu vichaa wanaotembea nusu uchi mitaani.
Watu wengi hawaelewi kuwa sisi ni sawa na watu wengine na kwamba sio wakati wote tunavaa nguo za ajabu.
na maisha tunayoishi siyo tofauti sana ya watu wengine. Ninaamka asubuhi, nakunywa chai
Nasugua meno, naoga, halafu naenda chuo ama kazini, na baadaye naenda nyumbani.
na siendeshi maisha maisha tofauti sana na ya watu wengine.
Lakini watu hawaelewi kwa sababu wengi wao wanajificha wakiogopa kuwa wazi kuhusu hili
... na kwa sababu ya ushawishi wa Saudi Arabia wanatuhumu …
Hello! Haya ni mahojiano. Unaweza kushiriki kama unataka.
- Umesikia alichosema? - Nini? - Hiki ni kipindi cha karaoke?