Tip:
Highlight text to annotate it
X
2.1 'Mwana wa Mungu' inamaanisha nini?
Maelezo kwamba Mwana wa Mungu yanamaanisha nini hasa?
Tunaelewa nini katika hilo?
Mungu,
Amezaa mtoto?
Astafurullah!!
Allah, ni mkuu mno,
ameinuliwa,
Allah’ ta’la,
yuko juu ya hayo,
Na kwakweli yeye mwenyewe hana mke
hakuna mwenzi wa maisha
hakuna mke
hii ni kama dhihaka.
hata kama ni kwa kufikiri kwa jinsi hiyo
Na Qur'an iko sahahihi kwa kusema hili,
na tunakubaliana nayo kabisa.
wenzetu walio wafuasi wa Masiha,
hawana shaka na hili,
hakuna ugomvi kabisa,
kwa kauli hiyo,
Makhtalafta,
hatupingani,
hapana.
Kwa ushuda wa maandiko ya awali, hakika,
Allah, hazai mtoto kama mwanadamu anavyozaa mtoto,
na mwanamke
Hivyo sivyo,
Maandiko yanavyofundisha.
Dhana ya MTOTO kwanza inaonekana katika ushuda wa Nabi Dawood,
Ni sura ya pili ya Zaburi,
ya Zabur,
tumeambiwa hukusu wadhifa maalum, aliopewa,
yule mtu ambaye Mungu amemchagua kumwakilisha,
kuwa mfalme juu ya Israel,
na katika maana fulani,
anamsimika kuwa caliph wake.
Na kwa habari ya kuongea kuhusu huyo mtu,
hasa katika mstari wa saba,
anasema leo,
leo,
Nimekufanya kuwa mwanangu.
Katika utamaduni wa siku hiyo,
wakati mfalme mkuu anaongea na kuonysha mahusiano na
wafalme wake wadogo,
mmoja wa wakilishi wake,
akitawala sehemu ya ufalme wake,
angemwongelea huyo bwana,
si tu kama mtumishi wake,
pia angetumia neno BWANA,
lakini,
mara nyingi,
uhusiano wa mfalme mkuu,
kwa mfalme huyo mwingine unaelezewa
kwamba ni uhusiano wa BABA' kwa Mtoto,
na mtoto kwa baba.
Na katika Zaburi hii kinatokea nini?
kuna dhana tatu zinawekwa katika dhana moja:
Yeye ni Masih,
ni mpakwa mafuta,
nimekupaka mafuta kuwa mfalme.
Wewe ni MFALAME,
wewe ni mwakilishi wangu,
wewe ni caliph (mtawala).
Na,
Zaidi ya hapo,
unaitwa MWANA.
Una mahusiano maalumu.
Yote matatu,
yamewekwa pamoja.
MASIHA,
MFALME,
MWANA.
Katika Kur'ani,
kwa mfano, katika suratul mumenin,
katika aya tisini na moja,
tunaambiwa kwa uwazi,
ku,
elewa kwamba hapana,
Allah HAKUZAA mtoto.
HAKUNA MTOTO,
aliyezaliwa na Allah.
Na inaendelea kueleza kwanini katika kurasa nyingine kwa mfano inatueleza ni kwa sababu
ni nani aliyempa mwenza,
mke?
Kuna maneno mawili kwa ajili ya Mwana katika Kiarabu.
La kwanza ni ibn (ابْنِ); na jingine ni walad (وَلَدً):
‘Ibn’ (ابْنِ) ni dhana pana inayoweza kuwa na maana nyingine,
isiyo ya kibaolojia.
Kur'ani yenyewe inaitumia dhana hii kwa maana nyingine
katika surat Baqara na aya 215,
ambapo wasafiri wanaitwa
ibn-alssabeeli, ابْنِ السَّبِيلِ,
au wana wa njia.
Kwa hiyo dhana hii ibn tafsiri sahihi ya Kiarabu
ya dhana ya Mwana iliyotumika,ni ile ya Yesu katika Biblia (‘υἱός’),
wakati 'Walad' (وَلَد) inamaanisha mwana aliyezaliwa kutokana na mahusiano ya kijinsia,
kama ilivyo kwa neno la Kiingreza offspring.
Hii ni dhana ya mahusiano,
walad,
ambalo Kur'ani inakataza,
si kwa maana ya ibn bali walad ambalo linamaanisha mwana wa kibaolojia.
Na kimsingi, tunapochambua mistari,
inakuwa dhahiri kwamba dhana ya 'mwana', ambayo Kur'ani inaikataa
si ile ambayo Injil inafundisha
isipokuwa ile yenye dhana ya dhihaka
kwamba, Allah alitwaa mke na akazaa mtoto kwa jinsi ya mwili
astafurullah!
Na kwa hiyo hakuna ukinzani
kati ya Kur'ani na Injil katika hili.
Ni jambo lilele moja.
Kinachoongelewa hapa siyo umwili,
kwani hilo limekatazwa,
bali kinachoongelewa hapa ni mahusiano maalum.