Tip:
Highlight text to annotate it
X
Kuna jambo moja kuhusu Zakir Naik
linalowafanya watu kufikiri
kwamba anajua anachokiongelea,
na ndipo hapo anapoweza kubadilisha ukweli,
sehemu mabalimbali,
na kwa haraka sana
kutoka kichwani kwake
katika namna ambayo inakufanya udhani kwamba,
lo, huyu mtu atakuwa na akili nyingi sana.
Lakini rafiki yangu mmoja alikaa chini
na kupitia mazungumzo yake ya dakika tano
na katika dakika tano hizo,
aliweza kufanya
zaidi ya makosa 25.
Charles Darwin alienda katika kisiwa kijulikanacho kama Keletropist
Hakuna kisiwa kama hicho cha
Keletropist popote.
Kimsingi kilikuwa ni kisiwa cha Galapagos
ambacho Darwin alitembelea
ambapo aliwakuta ndege aina ya 'finches'
na aliwakuta ndege wakidonoa magome.
Hawa ndege ''hawadonoi magome
kama Naik anavyosema.
Waliishi katika mazingira tofauti ya kiikolojia
Kwa kutokana na mazingira ya kiikolojia wanayo donoa,
midomo yao ilikuwa ikizidi kuwa mirefu au mifupi.
Tofauti alizoziona Darwin
katika ndege hawa
zilikuwa ni zaidi ya urefu wa midomo yao,
zilijumuisha tofauti za rangi,
ukubwa, tabia za kujamiiana
nyimbo,
na vyakula walivyopendelea.
Tofauti hizi zililinganishwa katika ndege wa jamii moja, si katika jamii tofauti.
Uchunguzi wa Darwin wa midomo inayotofautiana
ulifanyika katika aina kumi na nne tofauti za jamii za ndege
na si kwa aina moja tu kama anavyodai Dk Naik.
urefu wa mdomo kimsingi
haukutofautiana katika ndege wa jamii moja.
Charles Darwin alimwandikia barua rafiki yake, Thomas Thromtan,
Mawasiliano yote ya Darwin
yamechapishwa
na pia yanapatikana kwa njia ya kielektoniki
na hayana kumbukumbu
ya mtu yeyote aitwaye Thomas Thromtan,
Charles Darwin mwenyewe anasema kwamba kulikuwa kuna vitu vinakosekana,
hakukubaliana nayo,
Darwin alikubali kwamba kulikuwa kuna vitu vinakosena,
lakini hiyo haimaanishi
alipingana na kanuni yake mwenyewe-
kimsingi alibashiri ni wapi vitu vilikuwa vinakosekana.
sabau ni kwamba kama ukichambua kanisa,
kanisa lilikuwa kinyume na sayansi hapo awali.
Kanisa kamwe halikuwa kinyume na sayansi---
karibu wanasayansi wakubwa wote wa Ulaya
wa nyakati za Galileo,
akiwemo Galileo mwenyewe,
walikuwa Wakristo wa kweli.
Watu kama Newton, Copernicus, Kepler,
Boyle, Linnaeus, Pascal
wote walikuwa waumin wa kweli wa Biblia.
Na unakumbuka tukio la Galileo kuhukumiwa kifo;
walimhukumu Galileo adhabu ya kifo.
Galileo,
muumini wa kweli wa Kikatoloki,
hakuhukumiwa adhabu ya kifo.
Alihukumiwa kifungo cha maisha
siku ya Juni 21, 1633
kisha hukumu hiyo
ikapunguzwa na kuwa kifungo cha ndani.
Akafa miaka kumi baadaye
jioni ya January 8,
1642
akiwa mzee.
Galileo aliamini
kwamba, kanuni yake inaendana na Biblia,
na akaandika kitabu akielezea jambo hili
kwa kuzingatia tafsiri za awali
za Wakristo kama Augustine.
Naik anaendelea kutoa kauli ileile potofu
mara mbili zaidi,
lakini hebu tuchukulie kwamba ni kosa moja tu kuhusu ukweli.
Kwahiyo wanasayansi wote, wengi wao,
waliiunga mkono kanuni kwasababu ilikwenda kinyume na Biblia,
siyo kwasababu ilikuwa kweli.
Kimsingi, wanasayansi walio wengi
hawakuunga mkono kanuni ya Darwin
kwa miaka mingi,
na wengi wa wanasayansi hawa hawa
waliiheshimu Biblia.
Kimsingi,
habari hii ya Dk. Naik
ni mambo ya kutunga.
Hatua zote-kulikuwa na ''mabaki ya binadamu'' (homonites) manne
Kila kitu anachokisema Naik hapa si kweli.
Hakuna hilo neno ''mabaki ya binadamu'' (homonites).
Anapaswa kumaanisha 'hominids', yaani, wanyama watembeao kwa miguu miwili.
Wanasayansi wanatuambia leo kwamba, kulikuwa na ''mabaki ya binadamu'' manne (homonites).
Siyo kwamba kuna kuna jamii 'nne' za wanyama watembeao kwa miguu miwili,
ziko
angalau kumi na nne.
Kwanza ni Lucy pamoja na kijana wake [sic] Dosnopytichest,
Hakuna hao wanyama watembeao kwa miguu miwili wajulikanao kama ''dosnopytichest.''
Lucy alikuwa ni
Australopithecus afarensis', mnyama anayesadikiwa kuwa jamii ya binadamu wa kwanza,
aliyekufa takribani miaka milioni 3 na 1/2
zama hizi hazikuwa miaka milioni 3 na 1/2 iliyopita.
Ilikuwa ni kati ya mika milioni 1.6
na 10,000 iliyopita.
Kisha ikaja '*** sapiens' jamii inayoaminika kwamba mwanadamu wa sasa alitoka kwayo.
ambaye alikufa miaka elfu miatano tano iliyopita.
*** sapiens' hakufa miaka elfu mia tano ilyopita.
Mimi na wewe na hata Zakir Naik
ni jamii ya *** sapiens
Kisha akaja 'Neanderthal Man', jamii ya watu wa kale,
Kwa kuzingatia kanuni ya uibukaji wa mwanadamu
Neanderthal man' hakuwa
na uhusiano wa moja kwa moja na mwanadamu,
ila alitokea katika zama za 'ice-age', zama za barafu.
ambaye alikufa miaka mia mpaka miaka elfu arobaini iliyopita.
Neanderthal man' akatoweka
miaka elfu thelathini iliyopita,
siyo miaka ''mia mpaka miaka elfu arobaini iliyopita.
Kisha ikaja hatua ya nne, ya 'CroMagnon', mtu wa kale anayesadikiwa kuwa chanzo cha binadamu wa sasa;
CroMagnon' ni sawa na
*** Sapiens,
ambaye Naik alikuwa amemtaja
kama jamii ya zamani iliyo tofauti.
Hakuna uhusiano hata kidogo katika hatua hizi.
Kimsingi,
Wanabaolojia wa mabadiliko ya viumbe wameona mifano mingi
amabayo wanadai ina uhusiano
katika hatua hizi,
kwa mfano
*** habilis', jamii ya mtu wa kale
*** ergaster', jamii ya mtu wa kale
na '*** heidelbergensis', jamii ya mtu wa kale.
Kama unamfahamu Sir Albert Georgie,
aliyepata Tuzo ya Nobel kwa kugundua vitamin C,
Györgyi hakuvumbua Vitamin C, aligundua.
Vitamini C kwa asili ni kitu kinachotokea chenyewe
hakihitaji kuvumbuliwa.
Aliandika kitabu. The Crazy Ape and Man'' yaani ''Sokwe Mwendawazimu na Mtu dhidi ya kanuni ya Darwin.
Kitabu cha 'Albert Szent-Györgyi’ hakikuitwa
The Crazy Ape and Man''
ila kiliitwa
The Crazy Ape,
na kilikuwa hakipingani na mabadiliko
ila yalikuwa ni maoni ya kisosholojia.
Kama unamfahamu Ruperts Albert
Ruperts Albert ni nani?
Nashindwa kumpata mtu yeyote
anayezungumzia jina hilo.
Kama unafahamu kuhusu Whitemeat, Sir Whitemeat,
Whitemeat? Sir Whitemeat ni nani?
Kwa mara ya nne,
hakuna yeyote mwenye jina hili.
Katika ngazi za chini amiba katika jamii za chini za viumbe
amiba anaweza kubadilika na kuwa 'paremishia'.
Hakuna kitu kama “paremishia.
Pengine anamaanisha 'paramecium'.
Lakini badiliko la mabadiliko la amiba
kuwa 'paramecium'
ni suala linaloshangaza kibaolojia
kuliko kuliona kuwa ni dogo sana
tofauti ya kibaolojia kati ya sokwe na wanadamu
kulingana na Henses Crake ambaye ni mtaalamu katika eneo hili
alisema, halifikiriki.
Hakuna mtu ajulikanaye kama “Henses Crake.
Naik pengine anamaanisha Francis Crick,
ambaye ni mgunduzi-mwenza wa vinasaba.
Francis Crick anaamini kikamilifu katika mabadiliko.