Tip:
Highlight text to annotate it
X
Translator: David Mvoi Reviewer: Joachim Mangilima
Nyumbani, watu huniita mpiga makelele,
mleta matata, msumbufu,
muasi, mwanaharakati,
kioo cha jamii.
Lakini sikuwa hivyo.
Utotoni, nilikuwa na jina la utani.
Waliniita Softi,
yaani kijana mwepesi asiye na mambo mengi.
Kama binaadamu yeyote, niliepuka balaa,
Utotoni, walinifunza kimya.
Usibishane, fanya unachoambiwa.
Kwenye shule ya dini, walinifunza nisilete bughudha, nisibishane.
hata kama huna hatia, nyenyekea.
Hili lilisisitizwa na hali ya siasa.
(Kicheko)
Kenya ni nchi unayochukuliwa kuwa na hatia
hadi unapojulikana una mali
(Kicheko)
Wakenya maskini wanaweza mara tano zaidi
kupigwa risasi na polisi wanaopaswa kuwalinda
Kuliko wahalifu.
Haya yalisisitizwa na hali ya kisiasa nyakati hizo.
Tulikuwa na rais, Moi, aliyekuwa kiongozi wa kiimla.
Aliitawala nchi kwa mabavu,
na yeyote aliyethubutu kukiuka uongozi wake
alishikwa, akapigwa, akafungwa au kuuawa.
Hivyo wananchi walikuwa waoga werevu, kujiepusha na matata.
Kuwa mwoga halikuwa tusi.
Kuwa mwoga lilikuwa jambo zuri.
Tuliishi kuelezwa kuwa mtu mwoga hurudi nyumbani kwa mamaye.
Ilikuwa na maana hii: ukijiepusha na matata utaishi.
Niliushuku wosia huu,
na miaka minane iliyopita tukawa na uchaguzi nchini Kenya,
na matokeo yakapingwa vikali.
Kilichofuata kilikuwa fujo mbaya, ubakaji,
na mauaji ya zaidi ya watu elfu moja.
Kazi yangu ilikuwa kunasa fujo hizo.
Kama mnasa picha, nilinasa maelfu ya picha,
na baada ya miezi miwili,
wanasiasa hao walikutana, wakapata chai
wakatia sahihi mkataba wa amani na nchi ikasonga mbele.
Nilitatizika sana kwa sababu nilishuhudia rabsha kinaganaga
Niliona mauaji. Niliona waliofurushwa kutoka kwa makao yao.
Nilipata wanawake waliobakwa, na lilinitatiza,
lakini nchi kaikuyajali hayo.
Tulijidai. Tuligeuka kuwa waoga werevu.
Tuliamua kujiepusha na rabsha na kutojishughulisha.
Miezi kumi baadaye, niliacha kazi. Singeweza tena kustahimili hayo.
Baada ya kuiacha kazi, niliamua kujiunga na marafiki zangu
kuongea kuhusu ghasia nchini,
kuongeakuhusu hali taifa lilipokuwa,
na Juni Mosi Elfu mwaka wa Mbili na Tisa ilikuwa siku tuliyopanga kufika uwanjani
na kujaribu kupata sikio la rais.
Ilikuwa siku kuu,
sherehe yenyewe ilitangazwa kote nchini,
na nilifika uwanjani.
Marafiki zangu hawakutokea.
Nilijipata peke yangu,
na sikujua la kufanya.
Niliogopa,
lakini nilifahamu vyema kuwa siku hiyo,
Nilihitaji kufanya uamuzi.
Ningeweza kuishi kama mwoga, kama watu wengine,
au ningechukua msimamo thabiti?
Na rais aliposimama kuhutubu,
Nilijipata nimesimama nimkemea,
nikimwambia awakumbuke waasiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi,
kumaliza ufisadi.
Na punde si punde,
polisi walinirukia kama simba wenye njaa.
Walinifunga mdomo
na kuniburuta hadi nje ya uwanja,
ambapo walinitwanga na kunitupa jela.
Usiku huo nililala kwenye sakafu baridi ndani ya jela,
ndipo nikawaza.
Ni lipi lililonifanya nihisi hivyo?
Marafiki zangu na jamaa zangu walifikiri nimekuwa kichaa kwa yale niliyofanya,
na picha nilizonasa zilinisumbua.
Picha nilizonasa zilikuwa nambari tu kwa wakenya wengi.
Wakenya wengi hawakushuhudia ghasia.
Kwao ilikuwa hadithi tu.
Hivyo nikaamua kuanza maonyesho mtaani
kuonyesha picha za ghasia hizo nchini kote
na kuwapa watu fursa ya kujadiliana kuhusu ghasia hizo.
Tulizuru sehemu mbali mbali nchini na kuonyesha picha hizo,
na hio ilikuwa safari iliyoniweka katika mkondo wa uwanaharakati,
nilipoamua kutonyamaza tena kamwe,
Kuongea wazi kuhusu mambo yale.
Tulitembea na ugunduzi uliotokana na kuonyesha picha mitaani
ukachangia unanzilishi wa picha za kisiasa kuhusu hali iliyokumba nchi yetu,
kuongea kuhusu ufisadi, uongozi mbovu.
Hata tumefanya mazishi-ashiria.
Tumefikisha nguruwe kwenye bunge la Kenya
kuashiria tamaa ya wanasiasa
Hili limeigizwa nchini Uganda na nchi zingine,
na jambo kuu ni kwamba picha hizo zimechukuliwa na vyombo vya habari
na kusambazwa kote nchini, kote Africa.
Ingawa nilisimama peke yangu miaka saba iliyopita,
sasa nimekuwa mmoja katika jamii ya watu wanaosimama pamoja nami.
Simo peke yangu tena ninaposimama kuongea kuhusu mambo haya.
Mie ni mmoja kati ya kikundi cha vijana wanaopenda sana nchi yao,
wanaopania kuleta mabadiliko,
na hawaogopi tena, na si waoga werevu.
Hio ndio hadithi yangu.
Siku ile uwanjani,
Nilisimama kama mwoga mwerevu.
Kwa kitendo hicho kimoja, niliipungia mkono wa buriani miaka ishirini na nne ya kuishi kama mwoga.
Kuna siku mbili kuu zaidi maishani mwako:
ile siku uliyozaliwa, na ile utakapogundua kwa nini.
Siku ile niliposimama uwanjani nikikemea Rais,
Niligundua kwa kweli kwa nini nilizaliwa,
kwamba sitakimya tena nionapo unyanyasaji.
Je, wajua nia yako ya kuzaliwa?
Asanteni.
(Makofi)
Tom Rielly: Hadithi nzuri sana hii.
Nataka tu kukuuliza maswali machache.
Hii PAWA254:
umeunda studio, mahali vijana wanaweza kwenda
na kudhihirisha umuhimu wa vyombo vya utandawazi
kufanya mambo haya.
Ni yepi yanayoendelea na PAWA?
Boniface Mwangi: Tuna hii jamii ya watengeneza filamu,
wasanii, wanamuziki, na wakati kuna tukio nchini,
tunajiunga pamoja, tunajadiliana, na kulichukulia maanani tukio hilo.
Chombo muhimu zaidi kwetu ni sanaa,
kwa sababu tunaishi nyakati mabazo watu wanashughulika na mambo mengi maishani,
na hawana ule wakati wa kusoma.
Hivyo tunaeleza uwanaharakati na ujumbe wetu tukitumia sanaa.
Tukitumia muziki, usanii, sanaa, hayo ndiyo tufanyayo.
Naweza kusema jambo la ziada?
TR: Kwa kweli. (Makofi)
BM: Licha ya kutiwa mbaroni, kupigwa, kutishwa,
nilipogundua sauti yangu,
kuwa ningeweza kuchukua msimamo kwa lile nililoamini,
sina uoga tena.
Waliniita softi, lakini mie si softi tena,
kwa sababu niligundua mimi ni nani, yaani, kazi hio tu ndio nataka kufanya,
na ni raha ilioje kufanya kazi hio.
Hakuna jambo kuu kama kufahamu unapaswa kufanya jambo fulani,
kwa sababu hautakuwa na woga, unaendelea tu kuishi maisha kivyako.
Asanteni.
(Makofi)