Tip:
Highlight text to annotate it
X
Kwa kuchukua mwango wa uono ambao ni mbali na mawazo ya mababu zetu,
mitambo hii ya kitaalamu, darubini, inafungua njia ya kina na ya
uhakika wa kuelewa asili yetu- René Descartes, 1637
Kwa milenia na milenia binadamu alikuwa akizichunguza anga wakati wa usiku, wakati wa giza totoro.
bila kutambua nyota za galaxi yetu ya Njia ya Nyota (Milk Way galaxy) kama aina nyingine za jua.
au mabilioni ya “galaxi” ambazo huchangia katika Ulimwengu wetu
Au, kwani sisi ni vituo tu katika ulimwengu huu?
Ni hadithi ndefu ya mabilioni 13.7 ya miaka.
Tukiwa na macho yetu kama vifaa vya uchunguzi hatukuwa na njia nyingine ya.
kugundua mifumo ya sayari na jua kati ya nyota zingine au katika kudhihirisha.
kama kuna maisha nje ya ulimwmengu huu
Leo hii tuko katika njia ya kuweka wazi mengi ya
maajabu ya Ulimwengu, tukiishi kaitka muda wa ajabu sana
wa ugunduzi wa kiastronomia
Mimi ni DktJ na nitawaongoza katika maswala ya darubini -
chombo cha ajabu ambacho kilimsaidia binadamu katika kufungua.
mlango wa kuuelewa Ulimwengu.
MACHO ANGANI - Miaka 400 ya Uvumbuzi kwa Darubini
1. Mandhari mpya ya anga
Karne nne zilizopita, yaani mwaka 1609, mtu mmoja alitoka nje
katika mashamba yanayozunguka nyumba yake.
Alielekeza darubini yake duni katika mwezi, sayari na nyota.
Jina lake lilikuwa Galileo Galilei.
Na taaluma ya astronomia ikabadilika kabisa.
Leo, baada ya miaka 400 tangu Galileo aelekeze darubini yake angani
Wanaastronomia wanatumia vioo kabambe katika vilele vya milima kuchunguza anga.
Darubini za redio zinakusanya milio hafifu na minong’ono kutoka anga za mbali.
Wanasayansi wametuma darubini katika anga za mbali
juu ya vurugu za angahewa ya dunia yetu.
na mandahari imekuwa ni yakustaajabisha!
Hata hivyo Galileo, kusema kweli, hakugundua darubini.
Sifa hiyo inaelekwenda kwa Hans Lipperhey
Mdachi ambaye hakuwamashuhuri aliyejishughulisha na utengenezaji wa miwani
Lakini Hans Lipperhey hakuwahi kutumia darubini hiyo katika kuchunguza nyota.
Ila alifikiria kwamba ugunduzi wake huu ungesaidia zaidi.
mabaharia na wanjeshi.
Lipperhey alitoka katika mji mkubwa wa kibiashara ujulikanao kama Middelburg.
katika nchi iliyoshamiri ya Jamhuri ya Udachi
Katika mwaka 1608, Lipperhey aligundua kwamba wakati akiangalia vitu vilivyo mbali kwa
kwa kutumia lensi mbinuo(convex) na lens mbinuko (concave), kitu kinaweza kukuzwa, kama
lensi mbili zinawekwa katika umbali mwafaka kutoka lensi moja hadi nyingine.
Na Darubini ilizaliwa!
Katika Septemba ya 1608, Lipperhey alitangaza ugunduzi wake kwa
Prince Maurits wa Uholanzi
Asingeweza kuchagua wakati muafaka zaidi kwa sababu
wakati huo Uholanzi walikuwa katika migombano.
ya vita vya miaka 80 na Hispania
Darubini mpya hii ya kujasusi ilikuwa na uwezo wa kukuza vitu na kuonyesha.
meli za maadui yaliyo mbali mno kuonekana.
na macho pekee.
Ugunduzi wenye faida sana!
Hata hivyo serikali ya Udachi haikutambua ugunduzi wa Lipperhey na haikumpa haki milki kwa ugunduzi wa darubini.
Sababu yake ni kwamba wafanyabiashara wengine walidai kuwa ndio walioigundua.
hasa mshindani wa Lipperhey, Sacharias Jensen.
Ugomvi huo haujamalizika hadi leo.
Mpaka leo hii suala la ugunduzi wa darubini limebaki kitendawili.
Mwnaastronomia mtaliano, Galileo Galilei, muasisi wa fizikia ya kisasa
alisikia kuhusu ugunduzi wa darubini akaamua kutengeneza darubini yake mwenyewe.
Miezi kumi hivi iliyopita, habari zilivuma kwamba
M- Fleming ametengeneza kioo cha kijasusi (spy glass) ambacho kingetumika kuchunguza vitu.
hata vikiwa mbali na macho ya mwangaliaji viliweza
kuoneka kana kwamba viko karibu
Galileo alikuwa mwanasayansi mashuhuri wa muda wake.
Pia alikuwa akiunga mkono na kutetea mtazamo mpya wa kidunia uliokuwa ukiwakilishwa.
na mwanaastronomia Nicolaus Copernicus (kutoka Polandi) ambaye apendekeza kwamba .
Dunia inazunguka Jua na sio Jua kuzunguka Dunia.
Akiegemeza hoja zake katika aliyoyasikia kushusu darubini ya Kidachi, Galileo
alitengeneza darubini zake mwenyewe.
Zilikuwa za hali ya juu zaidi.
Mwishoni, bila kujali kiasi cha kazi na gharama, nikafanikiwa.
kujitengenzea darubini ya hali ya juu sana kiasi kwamba.
vitu vikiangaliwa katika darubini vilionekana karibu mara elfu moja.
kubwa kuliko vilivyoonekana kwaida kwa macho tu.
Sasa ulikuwa ni muda wa kuelekeza darubini yake angani.
Nimeelekea kuwa na maoni na kuamini kuwa sura.
ya mwezi siyo bapa na si mviringo hasa
kama kinavyoaminiwa na wanafalsafa wengi
lakini kina vinundu na ni kacha iliyojaa mashimo na miinuko.
siyo tofauti na ilivyo hapa Duniani.
Mandhari yenye mashimo, milima na mabonde.
Duniya kama ya kwetu!
Baada ya wiki chache, mnamo Januari 1610, Galileo aliangalia Mshtarii (Shumbula)
Jirani na sayari hiyo aliona ncha nne za mwanga zilizobadilisha.
nafasi zake usiku hadi usiku pamoja na Mshtarii
Ilikuwa kama minenguo ya pole pole ya vimwezi vinavyozunguka sayari hiyo.
Ncha hizi nne za mawanga zilikujakujulikana kama.
Miezi ya Galileo ya Mshtarii.
Je, Galileo aligundua nini zaidi?
Awamu za Zuhura!
Kama vile ya mwezi, sura ya Zuhura inaongezeka na kupungua kutoka hilali kwenda.
mwezi mpevu na kurejea tena kila mwezi.
Viungo vya ajabu pande mbili ya sayari ya Zohari.
Madoa meusi katika sura ya Jua.
Na kama kawaida nyota nyingi.
Kwa maelfu na hata mamilioni
kila moja ikiwa imefifia kiasi ambacho haziwezi kuonekana kwa macho pekee.
Ilikuwa kama kwamba wanadamu ghafla wametupilia mbali upofu wao.
Ulimwengu wote unasubiriwa kugunduliwa
Habari za ungunduzi wa darubini zilienea ulaya kama moto pori
Kutoka Prague, katika enzi ya Mfalme Rudolph II, Johannes Kepler .
Aliboresha darubini hiyo.
Huko Antwerp, mchoraji ramani Michael Van Langren alichora.
ramani za kwanza za kuaminika ya sura ya Mwezi, ikionyesha taswira yake alivyoamini ilivyo
ikiwa na makotinenti na mabahari
Na Johannes Hevelius, mfanyabiashara tajiri wa Poland alijenga
Darubini kubwa katika kituo cha kuangalia nyota iliyopo Danzig
Kituo hiki kilikuwa kikubwa sana kiasi cha kuenea mapaa ya majengo matatu.
Lakini vyombo bora zaidi vya wakati huo viliundwa .
na Christian Huygenes huko Uholanzi
Mwaka 1655, Huygens aligundua mwezi wa Titan ambao ni mwezi mkubwa kuliko zote katika sayari ya Zohari.
Baada ya miaka michache aligundua mfumo wa pete za Zohari
ambazo Galileo hakuweza kuzielewa kabisa.
Mwisho, Huygens aliona alama nyeusi na mng’aro
wa barafu katika ncha za kaskazini na kusini mwa sayari ya Meriki.
Je, kuna uwezekano wa kuwa na maisha katika sayari hii ya mbali na ya kiajinabi?
Swali hili linawashughulisha na wanaastronomia hadi leo.
Darubini za kwanza zilikuwa darubini ambazo zilitumia .
lenzi kwa ajili ya kukusanya pamoja mwanga wa nyota.
Baadae lenzi hizo zilibadilishwa na zile zakutumia vioo
Hizi darubini za kuakisi mwanga zilitengenezwa na Niccolo Zucchi
na baadae kuboreshwa na Isaac Newton
Sasa, katika karne ya 18 ni moja ya kioo kikubwa kupita vyote Duniani .
ambavyo vilitengenezwa na William Herschel, mwanamuziki aliyegeuka kuwa mwanaastronomia
ambaye alifanya kazi na dada yake Caroline
Nyumbani kwao Bath huko Uingereza wataalamu kakika familia ya Herschel waliweka chuma iliyoyeyushwa
Katika muundo maalum, na ilipopoa
walisugua uso wa chuma hadi kun’garisha kiais cha kuakisi mwanga wa nyota.
katika maisha yake yote Herschel aliunda zaidi ya darubini 400
Kubwa kuliko zote ilikuwa kubwa sana kiasi kwamba alihitaji wafanyakazi zaidi ya wane
kuzungusha kamba, magurudumu na nyenzo zote .
zilizohitajiwa kufuatilia mwendo wa nyota katika anga wakati wa usiku.
ambao kwa uhakika husababishwa na mzunguko wa dunia.
Sasa Herschel alikuwa kama mpima ardhi, alizipitia anga na.
kuorodhesha mamia ya mawingu katika anga za mbali na nyota mapacha.
Pia aligundua kwamba Njia ya Nyota (the Milky wWy) lazima ni bapa kama sahani
Na hata alipima mwendo wa mfumo wetu wa sayari na nyota kwa katika hiyo sahani ya Njia ya Nyota
kwa kuangalia mwendo wa wiano wa nyota na sayari.
Halafu tarehe 13 Machi, 1781 aligundua sayari mpya - Uranus
Hii ilikuwa miaka 200 kabla ya kurusha chombo cha anga cha NASA Voyager 2.
ambacho kiliwawezesha wanaastronomia kuchunguza kwa karibu dunia hiyo iliyo mbali sana na yetu.
katika nchi nzuri na yenye rtuba katikati ya Ireland, William Parsons.
mfalme wa tatu wa Rosse, alitengeneza darubini kubwa kuliko zote ya karne ya 19.
Darubini hii kuwa iliyokuwa na kioo cha chuma yenye ukubwa mkubwa wa mita 1.8 kwa upana, Darubini hiyo.
ilijulikana kama “The Leviathan of Parsonstown”
Usiku nadra zizizo na mawingu na mwezi angani, Earl alikaa na darubini
na kuvinjari anga za mbali katika Ulimwengu wetu.
Kwenye Wingu la Orion – sasa ijulikanayo kama kizazi cha nyota
Na kwenda kwenye maajabu ya Wingu la Kaa, mabaki ya mlipuko wa nyota (Supernova)
Na Wingu la Mzunguko?
Lord Rosse alikuwa wa kwanza kutambua umbo hilo.
Glaxi kama ya kwetu yenye mawingu na vumbi jeusi na gesi inayo ng’aa
mabilioni ya nyota na huwezi kujua –
sayari kama yetu ya Dunia.
Darubini imekuwa ni chombo chetu cha kuvumbua Ulimwengu wetu.